KOCHA Mkuu wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson,
juzi Alhamisi alikuwa kivutio kwenye Uwanja wa KC wakati wa mchezo wa
Ligi Kuu England dhidi ya Hull City kwa kukaa kwenye benchi la wachezaji
wa akiba huku akiwa ametinga sare za timu hiyo.

Kwenye mchezo huo, Manchester United iliduwazwa
kwa mabao mawili ya haraka, lakini uwepo wa Ferguson uliwatoa hofu
wachezaji na kocha wao, David Moyes na hivyo kupambana na kuibuka na
ushindi wa mabao 3-2 uliowafanya kupanda kwa nafasi moja kwenye msimamo
kutoka ya nane hadi namba saba.
Miamba hayo wa Old Trafford wanashika nafasi ya
saba kwenye msimamo, pointi nane nyuma ya vinara Arsenal wanaoongoza na
pointi zao 39.
0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!