Polisi ya Sudan imemtia mbaroni kiongozi mwingine wa upinzani nchini
humo. Ibrahim al-Sheikh mkuu wa chama cha Kongresi ya Sudan, ametiwa
mbaroni mapema leo huko katika jimbo la Kordofan Magharibi, nchini humo.
Ibrahim amekamatwa na polisi ya Sudan kwa tuhuma za kutoheshimu katiba,
kueneza propaganda za uongo na kutishia usalama wa taifa. Katibu wa
chama hicho, Abdelqayum Awad amesema kuwa, ikiwa tuhuma anazotuhumiwa
Ibrahim zitathibiti dhidi yake, basi kuna uwezekano wa kuhukumiwa adhabu
ya kifo. Itakumbukwa kuwa wiki tatu zilizopita, maafisa wa usalama wa
nchi hiyo, walimtia mbaroni Sadiq al-Mahdi, mkuu wa chama cha Umma
aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Sudan kwa tuhuma za uchochezi dhidi ya
serikali ya Rais Omar Hassan al-Bashir, suala lililopelekea wafuasi wa
kiongozi huyo kuandamana siku ya Ijumaa wakiishinikiza serikali ya
Khartoum kumuachilia huru kiongozi wao huyo.
Home »
siasa afrika
» HABARI KUTOKA SUDAN ZASEMA KUWA KIONGOZI MWINGINGE WA UPINZANI AMETUPWA GEREZANI
HABARI KUTOKA SUDAN ZASEMA KUWA KIONGOZI MWINGINGE WA UPINZANI AMETUPWA GEREZANI
Written By Unknown on Monday 9 June 2014 | Monday, June 09, 2014
Labels:
siasa afrika
0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!