Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » » HABARI KUTOKA LIBYA ZASEMA KUWA MAWAZIRI WA NCHI JIRANI NA NCHI HIYO WAKUTANA JIJINI CAIRO MISRI.

HABARI KUTOKA LIBYA ZASEMA KUWA MAWAZIRI WA NCHI JIRANI NA NCHI HIYO WAKUTANA JIJINI CAIRO MISRI.

Written By Unknown on Monday 25 August 2014 | Monday, August 25, 2014

Misri leo inatazamia kuwa mwenyeji wa kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Libya wa nchi jirani zake. Wizara ya Mambo ya Nje ya Libya imetangaza kuwa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Libya, Misri, Tunisia, Algeria, Sudan, Chad na Niger wanatazamiwa kushiriki katika kikao hicho cha Cairo.
Hapa ni Cairo nchini Misri...
Kundi hilo la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi hizo zilizotajwa mwezi uliopita lilifanya kikao na kutaka kufanyika mazungumzo ya kisiasa na kuundwa baraza la kufuatilia ufumbuzi wa mgogoro wa Libya. Hii ni katika hali ambayo, kundi la Fajr la huko Libya jana lilitangaza kuwa linadhibiti uwanja wa ndege wa kimataifa wa Tripoli.  Libya imekuwa ikikabiliwa na hali ya mchafukoge na mapigano ya ndani miaka mitatu baada ya kupinduliwa kiongozi wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi