Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » » HOFU YAANZA KUTANDA NCHINI BURUNDI BAADA YA TAARIFA ZA VIRUSI VYA EBOLA KUWASILI NCHINI D.R.C.

HOFU YAANZA KUTANDA NCHINI BURUNDI BAADA YA TAARIFA ZA VIRUSI VYA EBOLA KUWASILI NCHINI D.R.C.

Written By Unknown on Monday 25 August 2014 | Monday, August 25, 2014

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imethibitisha wagonjwa wawili wa wa kwanza kuambukizwa ugonjwa wa ebola nchini humo, na hivyo Kongo kuwa nchi ya tano ya Kiafrika kuthibitisha kesi za homa hiyo hatari. Felix Kabange Numbi Waziri wa Afya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema kuwa taasisi ya taifa ya utafiti wa kitiba ya nchi hiyo imethibitisha kuwa sampuli mbili za uchunguzi wa kimaabara za wagonjwa hao zimeonyesha kuwa watu hao wameambukizwa virusi vya homa hatari ya ebola.
Kabange amesema huo ni mlipuko wa saba wa homa ya ebola kuwahi kuikumba Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kwamba uzoefu ulioupata nchi hiyo katika milipuko sita iliyopita ya maradhi hayo, utatumika ili kukabiliana na maambukizo ya homa hiyo.
Shirika la Afya Duniani (WHO) jana lilisema kuwa mtaalamu wake wa magonjwa ya milipuko aliyekuwa ametumwa na shirika hilo huko magharibi mwa Afrika kwa minajili ya kutafuta njia za kukabiliana na mlipuko wa ebola ameambukizwa virusi vya ugonjwa huo. Hadi kufikia sasa watu 1427 wamefariki dunia kwa homa hatari ya ebola huko magharibi mwa Afrika.
   
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi