Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » » JE,ULIJUWA KILE AMBACHO SERIKALI YA LIBYA IMEOMBA KWA UMOJA WA MATAIFA (U.N)?BASI HIKI HAPA.

JE,ULIJUWA KILE AMBACHO SERIKALI YA LIBYA IMEOMBA KWA UMOJA WA MATAIFA (U.N)?BASI HIKI HAPA.

Written By Unknown on Thursday 14 August 2014 | Thursday, August 14, 2014

Bunge jipya la Libya limeuomba rasmi Umoja wa Mataifa uisaidie kukabiliana na machafuko. Bunge la Libya limeutaka Umoja wa Mataifa uingilie kijeshi ili kuwalinda raia na kurejesha utulivu nchini humo. Bunge la Libya pia limepiga kura ili kuwasambaratisha waasi, na kuwapa muda wa hadi mwishoni wa mwaka huu kujiunga na jeshi. Hatua hiyo imechukuliwa ili kuhitimisha machafuko nchini Libya.
Inafaa kukumbusha hapa kuwa, mji mkuu wa Libya, Tripoli umegeuka kitovu cha mashambulizi kati ya makundi hasimu ya wanamgambo, ambao wameweka ngome yao katika uwanja wa ndege wa mji huo uliofungwa tangu mgogoro uanze Julai 13 mwaka huu.
Kwa upande mwingine Jenerali msaatafu Khalifa Haftar amenzisha mashambulio mashariki mwa Libya, akitaka kuwasambaratisha wanamgambo.



TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi