Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » , » KAMA ULIKUWA HAUJUI HUYU NDIE RAIS SHUPAVU,SOMA VILE ALIVYO IKOSOWA JAMII YA KIMATAIFA KUHUSU MACHAFUKO YANAYO ENDELEA KUFANYWA NA ISRAEL KWA WAPALESTINA HUKO GAZA.

KAMA ULIKUWA HAUJUI HUYU NDIE RAIS SHUPAVU,SOMA VILE ALIVYO IKOSOWA JAMII YA KIMATAIFA KUHUSU MACHAFUKO YANAYO ENDELEA KUFANYWA NA ISRAEL KWA WAPALESTINA HUKO GAZA.

Written By Unknown on Wednesday 20 August 2014 | Wednesday, August 20, 2014

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amekosoa vikali kimya cha jamii ya kimataifa kuhusiana na mashambulio ya kinyama ya utawala haramu wa Israel pamoja na jinai za utawala huo dhidi ya wananchi wa Palestina. Rais Mugabe ambaye ni mwenyekiti wa kiduru wa Jumuiya ya Ustawi ya Kusini mwa Afrika SADC amebainisha kwamba, kimya cha jamii ya kimataifa kuhusiana na jinai hizo za Israel hakuna tofauti na kutenda jinai.  Rais Mugabe amesema, madola ya magharibi yanayojifanya kuwa vinara katika masuala ya maadili, haki za binadamu na wanadamu kamili yamekuwa watazamaji tu wa mauaji ya umati ya Israel dhidi ya wanawake na watoto wasio na hatia wa Palestina. Rais Mugabe wa Zimbabwe amesisitiza juu ya jumuiya ya SADC kufungamana na taifa la Palestina na kuongeza kuwa, imma Israel ni muhimu mno kwa Wamagharibi ndio maana hawawezi kuzuia jinai za utawala huo, au watoto wadogo wanaouawa kwa umati huko Gaza ni magaidi.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi