
Watu kadhaa wamejeruhiwa baada ya maroketi matatu yaliyorushwa na
makundi ya kigaidi ya Syria yanayoungwa mkono na nchi za kigeni kutua
huko Bekaa mashariki mwa Lebanon. Walid Sukkarieh jenerali mstaafu wa
jeshi la Lebanon amesema kuwa anaamini kuwa waasi wa Syria na waungaji
mkono wao ndio waliorusha maroketi hayo katika ardhi ya Lebanon. Maafisa
wa jeshi la Lebanon na wa harakati ya Hizbullah wamekagua eneo
lililoathiriwa na mashambulizi hayo ya maroketi ya magaidi wa Syria.
Nawar al Sahili mbunge wa harakati ya Hizbullah amesema kuwa siku zote
wanataraji mshambulizi ya maroketi kutoka Israel na si Syria na
kuwataarifu magaidi wa Syria kwamba, hawatishwi na uchokozi wao huo.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!