Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » » KAMA REAL MADRID ILIMSAJILI G.BALE IKIDHANI KWAMBA HILI TATIZO LA MGONGO NI TATIZO DOGO TU BASI ILIFANYA KOSA KUBWA:Dr A.Parajon

KAMA REAL MADRID ILIMSAJILI G.BALE IKIDHANI KWAMBA HILI TATIZO LA MGONGO NI TATIZO DOGO TU BASI ILIFANYA KOSA KUBWA:Dr A.Parajon

Written By Unknown on Thursday, 17 October 2013 | Thursday, October 17, 2013


MREMBO, Daniela Saurwald, ambaye ni mchumba wake hakuwepo hospitali sawa, lakini mama mzazi, Nancy, hakutaka kabisa kusubiri nyumbani.
Aliandamana na mumewe, Jorge, kumsindikiza mtoto wao Hospitali ya Northwestern Memorial huko Marekani. Daktari wa Real Madrid, Carlos Diez, alikuwepo na mwenzake wa timu ya taifa ya Argentina, Daniel Martinez, naye alikuwapo. Ni kutokana na uzito wa tatizo lililokuwa likimkabili mtu wao.
Daktari Fessler, ndiye aliyehusika kumpasua. Huyu ni Gonzalo Higuain, aliyelazimika kufanyiwa upasuaji misimu mitatu iliyopita kutokana na maumivu ya mgongo yaliyokuwa yakimsumbua na kutishia uhai wa soka lake.
Uzito wa maradhi yake ndio ulisababisha familia nzima ya Gonzalo kumsindikiza hospitali. Kocha Jose Mourinho akishinikiza afanyiwe upasuaji kwa sababu alimwonea huruma kutokana na hatima ya maisha ya soka la staa huyo wa Kiargentina walipokuwa pamoja Real Madrid.
Lakini, kwa sasa Gonzalo yupo Napoli kwenye Serie A na Mourinho amerudi Ligi Kuu England na kujiunga tena na Chelsea. Real Madrid imebaki na mkosi wake wa maradhi kama hayo kuwaandama wachezaji wake.
Agosti mwaka huu, Real Madrid, ilifanya kufuru baada ya kuvunja benki na kuandika historia mpya kwenye soka kwa kufanya usajili wa pesa nyingi zaidi duniani. Ni wakati walipomnasa winga wa Wales, Gareth Bale, kwa uhamisho wa Paundi 85 milioni.
Uhamisho ulikuwa gumzo Ulaya nzima na kuwafanya watu wengine wafike mbali na kuchambua mambo mengine ambayo yangeweza kufanywa kwa kutumia pesa hiyo ya usajili wa Bale.
Lakini hata mwaka ukiwa haujaisha, tayari Real Madrid inaonekana kama imeingia mkenge kwenye usajili huo uliowagharimu pesa nyingi.
Daktari asema Real Madrid imeliwa
Katika kusaka ukweli wa kitaalamu kuhusiana na maradhi ya mgongo yanayomsumbua Bale, gazeti maarufu jijini Madrid, MARCA lilifanya mahojiano na madaktari mbalimbali mahiri wa Kihispaniola.
Wakamfuata daktari mwenye hadhi kubwa, Avelino Parajon na akasema hivi: “Kama Real Madrid ilimsajili Gareth Bale ikidhani kwamba hili ni tatizo dogo tu, ilifanya kosa kubwa.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi