
Rais Rajoelina aliingia madarakani kwa kumpindua mpinzani wake wa karibu, Marc Ravalomanana ambaye amezuiliwa kugombea kwenye uchaguzi wa mwaka huu yeye pamoja na Rajoelina kufuatia shinikizo toka jumuiya ya kimataifa.
Kwenye kinyang'anyiro cha safari hii wagombea, Robinson Jean Louis atapambana na Hery Rajaonarimampianina kiongozi anayeungwa mkono na rais wa sasa Andry Rajoelina.
Katika uchaguzi wa duru ya kwanza Jean Louis alipata asilimia 21.16 ya kura zote na hivyo kuongoza kwenye awamu ya kwanza, kiongozi huyu anaungwa mkono na rais aliyeko uhamishoni, Marc Ravalomanana.
Wachambuzi wa mambo wanasema kuwa Louis ananafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huo kutokana na kupata uungwaji mkono mkubwa toka kwa vya vingine vya upinzani nchini humo.
0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!