Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » , » KAMA ULIKUWA HAUJUI BASI HIKI NDICHO ALICHO KISEMA CHRISTIANO RONALDO KUHUSIANA NA DI MARIA KUPEWA JEZI YA NAMBA YAKE YA ZAMANI.

KAMA ULIKUWA HAUJUI BASI HIKI NDICHO ALICHO KISEMA CHRISTIANO RONALDO KUHUSIANA NA DI MARIA KUPEWA JEZI YA NAMBA YAKE YA ZAMANI.

Written By Unknown on Friday 29 August 2014 | Friday, August 29, 2014

Mchezaji bora wa soka barani Ulaya Cristiano Ronaldo dos Santos Aveiro amemtakia kila la kheri mshambuliaji mpya wa klabu ya Man Utd Ángel Fabián Di María Hernández katika majukumu yake akiwa Old Trafford huko nchini Uingereza.
Ronaldo ambaye alitangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa barani Ulaya jana jioni kwa kuwashinda wapinzani wake Manuel Neuer pamoja na Arjen Robben amesema anatambua uwajibikaji wa Di Maria unaweza kufanya mageuzi makubwa katika kikosi cha Man Utd.
Lakini pamoja na kumtumia salamu za kumtakia kheri Ronaldo amemtaka Di Maria kuitendea mema jezi namba saba aliyokabidhiwa kwa kumueleza kwamba jezi hiyo ina majukumu makubwa.
Amesema wakati akisajiliwa Man utd mwaka 2003 alikabidhiwa jezi namba saba ambayo ulikuwa inatumiwa na gwiji wa soka nchini Uingereza David Robert Joseph Beckham na bila ajizi aliitendea mema kwa kufanya kusudio la kuibeba Man Utd wakati wote.
 
Hata hivyo Di Maria amekiri ni kweli alielezwa maneno hayo na Ronaldo na ameahidi kufanya jitihada za kutimiza kusudio la kuirejeshea fadhila jezi namba saba ya Man Utd.
Di Maria alitambulishwa rasmi kwa waandishi wa habari hapo jana.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi