Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » , » NEYMAR AANDIKA HISTORIA HII LA LIGA.

NEYMAR AANDIKA HISTORIA HII LA LIGA.

Written By Unknown on Tuesday 8 December 2015 | Tuesday, December 08, 2015

Historia imeandikwa leo ndani ya Jiji la Barcelona. Na Si Messi kama ilivyozoeleka bali ni mbrazil Neymar Dos Santos.  


Kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo, wameshuhudia mmoja wa wanasoka wake akitwaa tuzo ya mwanasoka bora wa La Liga wa mwezi. 
Mbrazil Neymar ndio aliyeileta tuzo hiyo Nou Camp kwa mara ya kwanza tangu ilipoanza kutolewa baada ya kutangazwa kuwa mwanasoka bora wa mwezi November wa La Liga. 
Neymar kwa sasa ndio mfungaji bora wa La Liga akiwa na magoli 14, na katika mwezi November pekee amefunga magoli matano katika mechi 3 za ligi hiyo. Villareal akiwafunga mara mbili, Madrid mara moja na Real Sociedad  akitikisa nyavu zao mara mbili.

NEYMAR

The La Liga Player of the Month Award ndio ipo katika mwaka wake wa pili tangu ilipoanza kutolewa. Msimu wa 2013/14  ndio ilitolewa kwa mara ya kwanza, na mpaka sasa imetolewa mara 21.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi