Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » , » CRISTIANO RONALDO ANA MAADUI WENGI:PAULO FUTRE

CRISTIANO RONALDO ANA MAADUI WENGI:PAULO FUTRE

Written By Unknown on Thursday 24 November 2016 | Thursday, November 24, 2016

Paulo Futre amesisitiza kuwa mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ana maadui wengi sana katika nchi yake, huku idadi kubwa ya raia wa nchi hiyo wakidaiwa kupenda Messi ashinde tuzo ya Ballon d’Or.
Ronaldo amejichimbia mizizi kwenye timu yake ya taifa ya Ureno na kuweka rekodi ya kipekee kwa nchi yake baada ya kuipa taji la Euro mwaka 2016.
Hata hivyo, Futre ambaye alicheza michezo 41 kwa nchi yake, anaamini kwamba Wareno wengi hawampendi Ronaldo kutokana na namna anavyojiweka katika maisha yake ya ndani na nje ya uwanja.
“Cristiano ni Mreno, amefanya kila kitu, ni bingwa wa Ulaya, lakini ana maadui wengi sana nchi Ureno kutokana na namna alivyo,” Futre alinukuliwa na SER.
“Huwa hapindishi ukweli wala hapendi kuzunguka na ndiyo maana anapata maadui wengi sana nchini mwake.. Mambo ambayo wakati mwingine huzungumza baada ya mechi na mtazamo wake ulivyo ndio tatizo kubwa sana.
“Kulikuwa na wakati watu walikuwa wanaimba Messi, Messi, Messi nje ya hoteli walikuwa wakiishi wachezaji wa timu ya Ureno, hali ambayo ilikuwa ni ya aibu mno.
“Bila shaka kuna watu nchini Ureno ambao wanataka Messi ashinde Ballon d’Or. Hiki ni kitu pekee kinachotokea Ureno.”

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi