KIUNGO mahiri wa 
kimataifa kutoka Ghana, Kevin Prince-Boateng amesisitiza kuwa Italia sio
 nchi ya kibaguzi pamoja na uhamisho wake kutoka AC Milan kwenda Schalke
 ya Ujerumani kuhusishwa na masuala hayo. Mapema
 mwezi huu bwana fedha wa klabu ya AC Milan, Peter Peters alikaririwa 
akidai kuwa uhamisho wa kiungo huyo ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na 
matukio ya kibaguzi yaliyokuwa yakimuandama mara kwa mara akiwa 
uwanjani. Lakini Boateng alikanusha tetesi hizo na kudai kuwa hakuondoka Milan kwa ajili ya matukio ya kibaguzi. Boateng
 amesema hakuondoka Italia kwa ajili ya wahuni wachache ambao wamekuwa 
wakiongoza vitendo vya kibaguzi na anaamini nchi hiyo sio ya kibaguzi 
kama watu wanavyofikiria. Mchezaji
 huyo amecheza Milan kwa misimu mitatu na kushinda taji moja la Serie A 
kabla ya kurejea nchini Ujerumani katika kipindi cha usajili wa majira 
ya kiangazi msimu huu. 
Home »
michezo ulaya
 » ITALIA SIO NCHI YA KIBAGUZI - BOATENG.
ITALIA SIO NCHI YA KIBAGUZI - BOATENG.
Written By Unknown on Thursday, 12 September 2013 | Thursday, September 12, 2013
Labels:
michezo ulaya



0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!