TIMU ya taifa ya Mexico 
inaweza kushindwa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia mwakani kwa mara ya 
kwanza baada ya kupita miaka 25 kama wakishindwa kushinda mechi zao 
mbili ambazo ndio zitaamua hatma yao. Hali
 imekuwa mbaya mpaka kufikia Shirikisho la Soka la Mexico kufikiria 
uwezekano wa kubadilisha kocha wa timu ya taifa ambaye anatakuwa watatu 
katika kipindi cha siku nne. Mbali
 na hivyo pia vyombo vya habari vimeonyesha mapenzi madogo kwa wachezaji
 baada ya kupoteza mchezo dhidi ya mahasimu wao Marekani kwa kufungwa 
mabao 2-0 huko jijini Columbus, Ohio Jumanne. Kupoteza
 mchezo dhidi ya Marekani kumekuja siku chache baada ya kupoteza mchezo 
mwingine dhidi ya Honduras Ijumaa iliyopita hivyo kupelekea Mexico 
kutupwa mpaka nafasi ya tano katika timu sita za kundi la CONCACAF. Katika
 kundi hilo timu tatu za juu ndio zitafuzu moja kwa moja kwenda Brazil 
huku timu ya nne itapelekwa kucheza hatua ya mtoano na New Zealand huku 
mpaka sasa zikiwa zimebaki nafasi mbili pekee baada ya Marekani na Costa
 Rica kufuzu kwa kuchukua nafasi mbili za juu.
Home »
michezo ulaya
 » MEXICO HATIHATI KUFUZU KOMBE LA DUNIA.
MEXICO HATIHATI KUFUZU KOMBE LA DUNIA.
Written By Unknown on Thursday, 12 September 2013 | Thursday, September 12, 2013
Labels:
michezo ulaya



0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!