KOCHA
Arsene Wenger amesema bao la kwanza la timu yake lililofungwa na Jack
Wilshere katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Norwich City lilikuwa moja ya
mabao bora aliyowahi kushuhudia katika miaka yake 17 ya kufanya kazi
katika klabu hiyo.
Wilshere
alimalizia bao zuri dakika ya 20 lililotoka na gonga safi, Arsenal
ikirejea kilelenimwa Ligi Kuu England, kabla ya Mesut Ozil kufunga
mawili na Aaron Ramsey moja.
Kabla
ya kufunga bao hilo linaloingia kwenye kinyang'anyiro cha bao bora la
msimu, Wilshere aligongeana pasi na Olivier Giroud kisha kumalizia kwa
kumtungua John Ruddy.
| . |
"Kweli
lilikuwa moja ya mabao bora na bao ambalo limelifrahia mno,"alisema
Wenger said. "Lilikuwa bao la timu na ilikuwa kasi ambayo unataka timu
yako icheze.
"Lilitokana
na mchanganyiko wa ubora wa ufundi na maamuzi ya haraka - lilikuwa babu
kubwa. Tumefunga mabao fulani mazuri msimu huu na yote manne yalikuwa
mazuri leo,".
| . |
| . |
| . |



0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!