Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » » RAIA 9 WA LEBANON MAHUJAJI AMBAO WALIKUWA WAMEKAMATWA SYRIA WAREJEA MJINI BEIRUT

RAIA 9 WA LEBANON MAHUJAJI AMBAO WALIKUWA WAMEKAMATWA SYRIA WAREJEA MJINI BEIRUT

Written By Unknown on Sunday, 20 October 2013 | Sunday, October 20, 2013

Mahujaji 9 raia wa Lebanon waliokuwa wakishikiliwa kama mateka nchini Syria wamewasili mjini Beirut baada ya kuachiwa kuru jana jumamosi, hatua hiyo imefikiwa baada ya makubaliano yaliyopelekea pia kuachiwa huru kwa Marubani wawili raia wa Uturuki waliokuwa wakishikiliwa kama mateka nchini Lebanoni.

Mahujaji hao toka katika dhehebu la kishia walipokelewa na Baraza la Mawaziri na Maofisa toka serikali ya Lebanon, familia zao nazo zilijumuika kuwalaki wapendwa wao walioonekana kuwa na afya njema ambao wameshikiliwa kama mateka kwa miezi kumi na saba.
Marubani wawili wa Uturuki Murat Akpinar and Murat Agca waliotekwa takribani miezi miwili iliyopita nao waliwasili mjini Istanbul jumamosi usiku na kulakiwa na familia zao pamoja na Waziri Mkuu Recep Teyyip Erdogan.
Marubani hao walishikiliwa na kundi ambalo lilitaka Uturuki itumie ushawishi wake kwa Syria ili iwaachie huru mahujaji 9 wa nchini Lebanon.


Makubaliano ya kuachiwa kwa mateka hayo yaliyohusisha pande tatu, yalikwenda sambamba na wito wa kuachiwa huru kwa wafungwa 200 wa Syria wanaoshikiliwa na utawala wa Rais Bashar al-Assad ingawa bado haijawekwa wazi kama Wasyria hao tayari wamekwishaachiwa huru.
Ndugu wa mahujaji wamekataa kuhusika na kupanga tukio la utekaji wa marubani ambao walitekwa katika eneo linalodhibitiwa na kundi la wapiganaji la Hezbollah, hata hivyo kiongozi mkuu wa kundi hilo Hassan Nasrallah amekanusha kuhusika na tukio hilo.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi