Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » » USHINDI WA CHAMA CHA RPG CHA RAIS ALPHA CONDE WA GUINEA WAPINGWA NA WAPINZANI

USHINDI WA CHAMA CHA RPG CHA RAIS ALPHA CONDE WA GUINEA WAPINGWA NA WAPINZANI

Written By Unknown on Sunday, 20 October 2013 | Sunday, October 20, 2013

Wapinzani nchini Guinea wanatarajia kwenda mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi wa wabunge yaliyotangazwa hivi karibuni ambayo yaliyokipa ushindi mkubwa chama tawala cha RPG kinachoongozwa na Rais wa nchi hiyo Alpha Conde.

Msemaji wa muungano wa wapinzani Sydia Toure amesema kamwe hawawezi kutambua matokeo ambayo hayawakilishi matakwa ya wananchi wa Taifa hilo.
Naye mpinzani mkuu wa Rais Conde toka chama cha UDFG Cellou Dalein Diallo amesema wana uthibitisho wa kutosha juu ya udanganyifu uliofanyika katika zoezi la uchaguzi.
Hatua hiyo ya wapinzani imezusha hofu kuwa huenda machafuko yakalikumba Taifa hilo lenye historia ya migogoro ya kisiasa na kijeshi na umwagaji damu kwa waandamanaji.
Mkuu wa Umoja wa Taifa katika mataifa ya Magharibi mwa Afrika, Said Djinnit ametoa wito kwa wapinzani kutafuta haki yao kwa kuzingatia misingi ya sheria na kuwa watulivu wakati wakisubiri maamuzi ya mahakama juu ya uhalali wa matokeo hayo.
Msemaji wa serikali Damantang Albert Camara amesema chama tawala kimeridhishwa na matokeo hayo ambayo yamehitimisha mchakato huo uliochukua muda mrefu kutamatika.
Hata hivyo waangalizi wa uchaguzi huo toka taasisi mbalimbali za kimataifa tarehe 9 ya mwezi huu walisema kulikuwa na dosari ngingi zinazoathiri uhalali wa matokeo ya uchaguzi huo.
Katika matokeo yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi siku ya ijumaa, chama tawala cha RPG pamoja na washirika vyama wake katika uchaguzi huo walipata jumla ya viti 70 kati ya viti 114 vya bunge zima, ambapo RPG pekee ilipata viti 53 na washirika wake walipata viti 7.
Chama pinzani cha UFDG kinachoongozwa na Cellou Dalein Diallo kilipata viti 37 wakati chama cha Waziri Mkuu wa zamani nchini humo Sidya Toure cha UFR kilipata viti 10 na nafasi nyingine zilizosalia zimekwenda kwa vyama vidogo vilivyoshiriki uchaguzi huo.
Matokeo hayo yametangazwa takribani majuma matatu baada ya zoezi la upigaji kura kufanyika, suala ambalo lilizidisha hofu kuwa huenda udanganyifu unafanyika ili kukipa ushindi chama tawala.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi