"Naamini watu zaidi ya milioni 3 watashiriki kwenye maandamano ya leo. Kama Yingluck hatajiuzulu, tutaendelea na maandamano, leo tunasimamisha mawasiliano ya barabarani kwa nusu siku, na safari nyingine tutasimamisha kwa siku nzima."
Lakini takwimu za polisi zimesema, idadi ya waandamanaji ilifikia laki 1.5.
Maandamano ya mara kwa mara yamekuwa yakishuhudiwa nchini
Thailand katika miezi miwili iliyopita. Hapo awali waziri mkuu Bibi
Yingluck alivunja bunge kujibu matakwa ya waandamanaji, na kutangaza
siku ya uchaguzi, lakini waandamanaji hawakuridhika na matokeo hayo na
kutaka Bibi Yingluck mwenyewe kujiuzulu na kuahirisha uchaguzi
uliopangwa kufanyika mwezi Februari mwakani ili kupata muda wa mwaka
mmoja na nusu wa kujindaa kwa uchaguzi mkuu na kufanya mageuzi.
"Tumeamua kutoshiriki kwenye uchaguzi wa mwakani. Ningependa kuwaambia wananchi wanaotaka kukipigia kura chama cha Demokrasia, kwamba mageuzi ambayo mngependa kuyaona yatatimizwa, na siku hiyo itakapofika, tutafanya mageuzi ya muda mrefu na kurudisha imani ya wananchi juu ya demokrasia na mfumo wa bunge. Haya ndiyo matumaini ya chama cha Demokrasia. Tumefanya uamuzi huu na tutaendelea nao."



0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!