Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » » BREAKING NEWS...BREAKING NEWS...NAHODHA WA TIMU YA MAN-UTD NEMANJA VIDIC ATANGAZA KUONDOKA OLD TRAFFORD

BREAKING NEWS...BREAKING NEWS...NAHODHA WA TIMU YA MAN-UTD NEMANJA VIDIC ATANGAZA KUONDOKA OLD TRAFFORD

Written By Unknown on Friday, 7 February 2014 | Friday, February 07, 2014

NAHODHA wa klabu ya Manchester United Nemanja Vidic amebainisha kuwa anatarajia kuondoka mwishoni mwa msimu huu. Beki huyo wa kimataifa wa Serbia ambaye mkataba wake unaisha kiangazi, alianza kuitumikia United mwaka 2006. Vidic aliiambia tovuti ya klabu hiyo kuwa hana mpango wowote wa kucheza katika timu yoyote nchini Uingereza kwani timu pekee aliyokuwa akitaka kuichezea ilikuwa Manchester United.

Nyota huyo amesema ni jambo ambalo hakulitegemea kushinda mataji 15 akiwa hapo, hata hivyo ameamua kuondoka msimu huu ili kutafuta changamoto mpya sehemu nyingine. Vidic ambaye alinunuliwa kwa paundi milioni 7 kutoka klabu ya Spartak Moscow alitua rasmi United katika siku ya Christmas mwaka 2005, alikuwa nahodha wakati United ikishinda taji lake la 20 la Ligi Kuu huku kwa upande wake ilikiwa la tano chini ya Sir Alex Ferguson.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi