Rais wa
Marekani Barack Obama amepongeza jitihada zinazofanywa na Serikali ya
Ufaransa katika kusimamia upatikanaji wa amani na usalama wa dunia
ikiwa ni pamoja na kupambana na vitendo vya kigaidi .Rais Obama amesema
Ufaransa chini ya utawala wa Rais Francois Hollande imeonyesha ujasiri
katika hatua za kushughulikia migogoro inayozikumba nchi mbalimbali
duniani.
Katika mkutano wa pamoja wa na vyombo vya habari, ma rais hao
wamepongezana kuhusu kudumisha mahusiano ya kihistoria wapofikia katika
ushirikiano licha ya kuwepo kwa mambo kadhaa ambayo yamekuwa
yakiwatofautisha.
Obama ameeleza kuwa ufaransa imejitoa kwa dhati kwenye migogoro ya
nchi za Syria, Mali na Jamhuri ya Afrika ya Kati na changamoto
inayotokana na mpango wa nyuklia wa nchi ya Iran amabayo imekuwa katika
mvutano mkali na mataifa yenye nguvu duniani.
Katika hatua nyingine rais huyo wa marekani amesema kuwa Marekani itaendelea kuwa na ushirikiano mzuri na nchi za ulaya bila kubagua kwa kuwa nchi zote ni muhimu.
Kwa upande wake rais Francois Hollande amesema kuwa Ufaransa itaendelea kutoa ushirikiano kwa Marekani ili kushughulikia masuala yanayohusu amani, usalama na vita dhidi ya vitendo vya kigaidi.
katika hatuwa nyingine Rais wa Marekani Barack Obama ametowa
tahadhari kwa makampuni ya Ufaransa yanayo kwenda Iran kufanya biashara
na taifa hilo wakati huu muafaka juu ya mpango wa Nyuklia wa Iran
haujapatikana. Kauli hii ya Obama inakuja wakati huu makampuni ya
Ufaransa yamekuwa yakielekea Iran kwa ajili ya mpango wa kuanzisha
biashara na taifa hilo.
Mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka jana, serikali ya Iran na mataifa sita yenye nguvu duniani ikiwa ni pamoja na China, Marekani, Ufaransa, Uingereza, Urusi na Ujerumani walifikia muafaka wa miezi sita huku Iran ikikubali kupunguza urutubishwaji wa Nyuklia, na hivo kupunguziwa pia vikwazo vya kiuchumi.

Katika hatua nyingine rais huyo wa marekani amesema kuwa Marekani itaendelea kuwa na ushirikiano mzuri na nchi za ulaya bila kubagua kwa kuwa nchi zote ni muhimu.
Kwa upande wake rais Francois Hollande amesema kuwa Ufaransa itaendelea kutoa ushirikiano kwa Marekani ili kushughulikia masuala yanayohusu amani, usalama na vita dhidi ya vitendo vya kigaidi.

Mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka jana, serikali ya Iran na mataifa sita yenye nguvu duniani ikiwa ni pamoja na China, Marekani, Ufaransa, Uingereza, Urusi na Ujerumani walifikia muafaka wa miezi sita huku Iran ikikubali kupunguza urutubishwaji wa Nyuklia, na hivo kupunguziwa pia vikwazo vya kiuchumi.
0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!