Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » , » HABARI KUTOKA UTURUKI ZASEMA KUWA WACHIMBA MIGODI 200 NA ZAIDI WAFARIKI DUNIA NA WENGINE HAWAJUI WALIKO BAADA YA MRIPUKO KUTOKEA.

HABARI KUTOKA UTURUKI ZASEMA KUWA WACHIMBA MIGODI 200 NA ZAIDI WAFARIKI DUNIA NA WENGINE HAWAJUI WALIKO BAADA YA MRIPUKO KUTOKEA.

Written By Unknown on Wednesday, 14 May 2014 | Wednesday, May 14, 2014

Habari kutoka Uturuki zinasema kuwa, takriban wachimba migodi 201 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 200 hawajulikani waliko kufuatia mlipuko mkubwa uliotokea kwenye mgodi wa mkaa katika mkoa wa Manisa ulioko magharibi mwa nchi hiyo. Habari zaidi zinasema kuwa zaidi ya watu 500 walikuwa kwenye mgodi huo wakati mripuko ulipotokea jioni ya jana. Meya wa jimbo la Manisa, Cengiz Ergun, amesema idadi ya vifo inatarajiwa kupanda kwani wachimba migodi wengi bado wamefukiwa kwenye mgodi huo hadi sasa. Baadhi ya mashuhuda wanasema walisikia mripuko mkubwa na kisha baadaye wakaona moto mkubwa kwenye mgodi wa mkaa wa Manisa. Hadi tunakwenda hewani takriban watu 50 walikuwa wameokolewa na shughuli za uokoaji bado zinaendelea. Waziri Mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan amevunja safari yake ya Albania na anatarajiwa kuwasili Manisa leo Jumatano.
Ajali mbaya zaidi kwenye migodi ya Uturuki kuwahi kushuhudiwa katika miaka ya hivi karibuni ni ile ya mwaka 1992 ambapo wachimba migodi 263 walipoteza maisha baada ya kutokea mripuko kwenye mgodi mkubwa katika eneo la Zonguldak.

Hizi ni picha kadhaa za tukio:

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi