Maafisa wa usalama katika pwani ya Libya wamewakamata wahamiaji
haramu 114 kutoka nchi za Kiafrika ambao walikuwa wamejazana ndani ya
boti moja ndogo wakielekea bara Ulaya.
Maafisa wa Gadi ya Ulinzi ya Pwani ya Libya walisema jana Alkhamisi kuwa waliwakamata wahajiri hao haramu karibu na eneo la Gharbouli mashariki mwa Tripoli. Imedokezwa kuwa wahajiri hao waliokamatwa ni kutoka nchi za eneo la kusini mwa jangwa la Sahara barani Afrika hasa kutoka Senegal. Aghalabu ya wahajiri hao haramu huingia Libya kupitia mipaka ya kusini mwa nchi hiyo ambapo ina mipaka ya pamoja na Sudan, Chad, Nigeri na Algeria. Mwaka huu pekee wahamiaji 43,000 wameingia Italia wakitokea eneo la Kaskazini mwa Afrika hasa Libya. Njia ya Libya inatumiwa na wahamiaji hao kutokana na ghasia zinazoendelea nchini humo ambazo zimepelekea serikali kushindwa kuidhibiti ipasavyo mipaka ya nchi kavu na baharini.
Maafisa wa Gadi ya Ulinzi ya Pwani ya Libya walisema jana Alkhamisi kuwa waliwakamata wahajiri hao haramu karibu na eneo la Gharbouli mashariki mwa Tripoli. Imedokezwa kuwa wahajiri hao waliokamatwa ni kutoka nchi za eneo la kusini mwa jangwa la Sahara barani Afrika hasa kutoka Senegal. Aghalabu ya wahajiri hao haramu huingia Libya kupitia mipaka ya kusini mwa nchi hiyo ambapo ina mipaka ya pamoja na Sudan, Chad, Nigeri na Algeria. Mwaka huu pekee wahamiaji 43,000 wameingia Italia wakitokea eneo la Kaskazini mwa Afrika hasa Libya. Njia ya Libya inatumiwa na wahamiaji hao kutokana na ghasia zinazoendelea nchini humo ambazo zimepelekea serikali kushindwa kuidhibiti ipasavyo mipaka ya nchi kavu na baharini.
0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!