Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » » ALICHO KISEMA ADNAN JANUZAJ BAADA YA KUONGEZA MKATABA KUENDELEA KUICHEZEA MAN UTD CHINI YA D.MOYES

ALICHO KISEMA ADNAN JANUZAJ BAADA YA KUONGEZA MKATABA KUENDELEA KUICHEZEA MAN UTD CHINI YA D.MOYES

Written By Unknown on Sunday, 20 October 2013 | Sunday, October 20, 2013


Klabu ya Manchester United imethibitisha kuwa winga mzaliwa wa Belgium,Adnan Januzaj amesaini mkataba wa miaka mitano wa kuwatumikia mabingwa hao watetezi.
Chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 18 ambaye alianza vizuri Ligi Kuu ya Uingereza kwa kufunga goli mbili katika mchezo wake wa kwanza amejifunga kwa mashetani hao wekundu mpaka mwaka 2018.

Januzaj asaini miaka mitano Old Trafford.

Meneja wa Man United,David Moyes amesema kuwa amefarijika sana kuona Adnan kaamua kujifunga na kutafutia mafanikio klabuni hapo.Akidai kuwa ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa na amempa matumaini makubwa tangu awasili kuinoa klabu hiyo mwezi Julai.
.
Huku akiongeza kuwa Old Trafford ni mahala pazuri kwake kwa kutafuta mafanikio na kuendeleza kipaji chake kwani pana utamaduni mzuri wa kuwajali wachezaji chipukizi na kuwapa nafasi kwa kiasi kikubwa.
Januzaj alisisitiza kuwa ni hatua kubwa kwake kusaini Manchester United.Pia akadai tangu awasili hapo mara nyingi alikuwa akiwaza jambo hilo na kusema klabu hiyo ni chagua lake sahihi.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi