Katika siku kama ya leo miaka 558 iliyopita, iliyopita kazi ya 
uchapishaji vitabu ilianza na kitabu cha kwanza kabisa kikachapishwa kwa
 kutumia mashine iliyogunduliwa na Mjerumani Johannes Gutenberg. Mashine
 hiyo ya uchapishaji ilikuwa hatua muhimu katika njia ya uchapishaji na 
uenezaji wa elimu na maarifa kati ya wanadamu. Katika zama zake, 
Johannes Gutenberg pia alichapisha kitabu cha Biblia maarufu kwa jina 
la' Gutenberg Bible.' Hii leo kurasa kadhaa zilizobakia za kitabu hicho 
zinahifadhiwa katika jumba la makumbusho.
***
Siku kama ya jana miaka 143 iliyopita vijidudu maradhi 
vinavyosababisha maradhi ya ukoma viligunduliwa na tabibu na mhakiki wa 
Norway kwa jina la Gerhard Henrik Armauer Hansen. Ugonjwa huo huambatana
 na vidonda vikali vinavyovuruga na kuharibu maumbo ya muathirika. 
Vijidudu maradhi vya ugonjwa huo wa ukoma pia hukusanyika katika mishipa
 ya neva na kusababisha uharibifu katika sehemu kubwa ya mishipa ya 
neva. Maradhi hayo hujitokeza zaidi katika maeneo yenye joto. Licha ya 
maendeleo makubwa ya kisayansi yaliyopatikana katika kudhibiti ugonjwa 
wa ukoma, lakini njia ya kutibu maradhi hayo sugu bado haijapatikana na 
kuna idadi kubwa ya waathirika wake wanaendelea kuteseka katika nchi 
mbalimbali duniani.
***
Siku  kama ya jana miaka 7 iliyopita Harakati ya Mapambano ya Kiislamu
 ya Palestina HAMAS  ilipata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa Bunge 
ikiwa ni mara ya kwanza kwa harakati hiyo kushiriki kwenye zoezi hilo. 
Katika uchaguzi huo uliosimamiwa na waangalizi wa kigeni, Hamas 
ilifanikiwa kupata viti 76 kati ya jumla viti 132 vya Bunge la Palestina
 licha ya propaganda chafu zilizokuwa zikifanywa na vyombo vya habari 
vya nchi za Magharibi. Kwa utaratibu huo Hamas ilimuarifisha Ismail 
Hania kama Waziri Mkuu na kutangaza kwamba itaunda serikali ya umoja wa 
kitaifa. Hata hivyo nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani na 
muitifaki wake Israel, zilikataa kutambua rasmi serikali hiyo 
iliyochaguliwa kidemokrasia na wananchi wa Palestina.



0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!