David
 Moyes alimsaini Juan Mata kutoka akiwa na matumaini na mategemeo 
makubwa. Juan Mata alionekana kama mtu atakayekuja kuleta mageuzi ya 
kuisadia timu hiyo kuingia hata kwenye Top 4. Hata hivyo hali imekuwa 
tofauti na matarajio, Manchester United ikishinda mchezo mmoja tu kati 
ya minne Mata aliyocheza. Moja ya vitu vinavyoachangia matatizo haya ni 
mbinu za kiufundi, hivyo je inafaa kwa Moyes kuangalia upya mbinu zake 
ili kupata matokeo mazuri kutoka kwa mchezaji wake wa gharama zaidi - 
Juan Mata? 
Mahala aambapo amekuwa akichezeshwa Mata. 
Baadhi
 ya watu walihisi Moyes angebadili mfumo kwenda kutumia 4-2-3-1 ili 
kuweza kupata matokeo mazuri kutoka kwa Wayne Rooney, Mata na Adnan 
Januzaj nyuma ya mshambuliaji wa mbele Robin van Persie, ingawa hilo 
halijawezekana mpaka sasa. Mata amekuwa akichezeshwa kama kiungo wa 
kulia au kushoto. Dhidi ya Arsenal alichezeshwa kama kiungo wa kushoto, 
ingawa alijaribu kuingia ndani ili kuwa karibu na washambuliaji wawili 
wa mbele 
| . | 
Kama
 mchoro wa picha unavyoonesha hapo juu, United walikuwa wanacheza na 
Arsenal inayogombea ubingwa ugenini, lakini hapo juu tunaona Mata 
alitumia muda mwingi katika maeneo ya ulinzi, akikaa sana nyuma katika 
eneo la kulinda zaidi lango la timu yake (kutokea kushoto pia). Huu 
mfumo kwa hakika huwezi kukupa matunda mazuri kutoka Mata ambaye anakuwa
 bora zaidi anapokuwa na mpira miguuni mwake. Ndio maana haishangazi 
kuona Mata hakuwa na mchezo mzuri siku hiyo, akitengeneza nafasi mbili 
tu kwa Van Persie. 
Dhidi
 ya Fulham alicheza vizuri kiasi na kuwa na mpira muda mwingi, ingawa 
alifanya hivi akicheza kwenye winga ya kulia katika mchezo ambao 
ulitawaliwa na krosi kutoka kwa wachezaji wa kikosi cha Moyes. Man 
United ilijaribu kupiga krosi 82, staili ambayo sio tu imepitwa na 
wakati lakini pia ni staili ambayo ndani yake huwezi kuona ubora wa Juan
 Mata, ambaye hufanya vizuri kazi yake anapocheza katikati ya mistari ya
 safu ya ulinzi na kiungo, na sio pembeni. 
Mahala kwa kubadilisha
Mata
 hakufanya vibaya dhidi ya Fulham, alitengeneza nafasi tano za kufunga 
kwa wachezaji wenzie na katika mechi nne alizocheza ametengeneza jumla 
ya nafasi 13 (namba ya nafasi alizotengeneza Ashley Young msimu mzima). 
Lakini angeweza kufanya vizuri zaidi. Dhidi ya Fulham alikuwa na mpira 
kwa muda mwingi na alikamilisha 96% ya pasi zake zote.
| . | 
Lakini
 tatizo pekee la hizo pasi zilikuwa katika maeneo ya pembeni, hasa 
upande wa kulia. Haya sio maeneo ya kupata ubora wa Mata. Mata anahitaji
 kuchezeshwa kati kati ya safu ya ulinzi ya wapinzania na kiungo, mahala
 ambapo anaweza kutumia jicho lake la pasi nzuri kwenda kwa 
washambuliaji. Kama tunavyoona kwenye picha hapo juu, hakuwa na mamalka 
ya mchezo kwenye eneo hilo. 
Wazo
 la kwanza mbadala na kumuondoa mshambuliaji mmoja na kumchezesha Mata 
namba 10, jambo litakalomfanya awe na mpira muda mrefu na kuutumia 
katika maeneo ambayo anataka, sio kurudi nyuma kama ambavyo alivyokuwa 
akifanya dhidi ya Arsenal. Alicheza kwenye eneo hili katika mchezo pekee
 wa ushindi wa United katika mechi nne zilizopita - mechi dhdi ya 
Cardiff, ambapo alitengeneza nafasi nne.
Moyes
 anaonekana hataki au anasita kuwatumia Januzaj, Mata na Rooney katika 
kikosi kimoja na Van Persie. Hii inawezakana inatokana kwamba wachezaji 
wake wote watatu wa zamani wana uwezo wa kuingia ndani nyuma ya 
mshambuliaji wa kati. Njia pekee ya kufanya mfumo huu kufanya kazi ni 
kuachana na mfumo wa krosi na kuachia mpira wa pasi zaidi kuelekea ndani
 utumike zaidi.
Hitimisho
Hivi
 sasa David Moyes hapati matunda bora ya Juan Mata. Mfumo wa kutumia 
krosi ambayo Mata anatumika katika winga sio mzuri katika kutaka kupata 
matunda ya Juan Mata. Mata anahitaji uhuru wa kufanya kazi yake katika 
maeneo yake ya kati ya uwanja, hasa kwenye eneo la nyuma ya 
mshambuliaji. Ikiwa Moyes atabadili mfumo kwenda 4-2-3-1 ambao unamfiti 
Mata, Januzaj na Rooney wakicheza nyuma ya Van Persie. Jambo pekee la 
kuzingatia ni kuhakikisha mabeki wa pembeni wanakuwa na uwezo wa kutoa 
msaada mkubwa wakati timu inaposhambuliwa. Moyes hana cha kupoteza hivi 
sasa - hasa baada ya mfumo wa sasa wa 4-4-2 kutokuwa na matunda kwa timu
 na kupelekea matokeo mabaya. 



0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!