Beki wa Manchester City,Pablo Zabaleta 
amemtuhumu mwamuzi kutoka Ufaransa,Stephane Lannoy kwa maamuzi yake ya 
kushtusha dhidi yake katika mchezo waliofungwa 2-1 na Barcelona.
Raia huyo wa Argentina,alitolewa nje katika 
uwanja wa Nou Camp kufuatia kupewa kadi mbili za njano,huku kadi ya pili
 ikionyeshwa mara baada ya kumzonga Lannoy kuhoji kwanini alishindwa 
kutoa adhabu ya penati kufuatia Edin Dzeko kufanyiwa faulo na Gerard 
Pique kwenye eneo la hatari.
Barcelona pia walistahili kupewa penati halali
 wakati Messi alipoangeshwa katika eneo la hatari na Lescott katika 
kipindi cha kwanza huku wakinyimwa pia goli kwa madai walikuwa wameotea 
wakati marudio ya picha za video zilionyesha wazi kuwa Jordi Alba 
alikuwa eneo sahihi wakati akitoa klosi kwa Neymar ambaye aliukwamisha 
mpira wavuni.
Zabaleta alikuwa anaamini Man City walistahili
 kupewa penati kwa madhambi aliyofanyiwa Dzeko na anadai kuwa yupo 
gizani kwa kutokufahamu kwanini alitolewa nje na mwamuzi.
Huku akisisitiza,”Ilikuwa wazi sana.Nafikiri 
Pique alikuwa nyuma yangu na alifanya ukabaji mbaya kwa Dzeko na 
kumwangusha chini huku mwamuzi akiwa mita mbili kutoka mahali 
lilipotokea tukio hilo.”
Na kuongeza kuwa,”Sifahamu kwanini nilitolewa nje.Nilienda kwake kuongea naye kwa njia ya utaratibu kabisa.”
Pia akakiri kuwa alikuwa na hasira sana kwa mwamuzi huyo kwasababu hakuwapa penati lakini mara zote maekuwa akimuheshimu sana.
Lakini alisisitiza kuwa ameumizwa na 
kusikitishwa sana kwani anafikiri ulikuwa uwamuzi wa kushtusha 
sana.Akiongeza kuwa mara nyingine katika mchezo wanakuwa na wasiwasi na 
presha kwasababu wanakuwa wanajaribu kupata matokeo mazuri na maamuzi 
mabaya ya refa huwapa hasira sana.
Zabaleta akaongeza kuwa anahisi Man City 
walistahili kupewa faulo kutokana na Dzeko kufanyiwa faulo sekunde 
chache kabla ya Messi kufunga goli.
Mwisho akathibitisha hasira zake na masikitiko
 yake lakini akatoa pongezi kwa timu yake kwasababu anafikiri walicheza 
mpira wa kiwango cha juu sana kwani walianza mchezo vizuri na kumaliza 
vizuri na walikuwa na uwezo wa kufunga mwanzo na walikuwa na nafasi 
nyingine kadhaa.



0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!