Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » , , » KAMA ULIKUWA HAUJUI BASI HIKI NDICHO KILICHO MFANYA ASHLEY COLE AACHANA NA CLUB YA CHELSEA NA KUJIUNGA NA CLUB YA AS ROMA.

KAMA ULIKUWA HAUJUI BASI HIKI NDICHO KILICHO MFANYA ASHLEY COLE AACHANA NA CLUB YA CHELSEA NA KUJIUNGA NA CLUB YA AS ROMA.

Written By Unknown on Wednesday, 16 July 2014 | Wednesday, July 16, 2014

Beki wa pembeni kutoka nchini Uingereza Ashley Cole, ameweka hadharani kinaga ubaga kilichompeleka nchini Italia kujiunga na klabu ya AS Roma.
Cole, ambaye alikuwa mchezaji wa klabu ya Chelsea kuanzia mwaka 2006 amesema aliamini soka lake lingeishia nchini Uingereza, lakini mambo yamebadilika na leo amejikuta yupo nje ya nyumbani.
Cole, amesema wakala wake ndio chanzo cha kukubali kuondoka jijini London na kwenda jijini Roma, kutokana na mambo mazuri aliyomueleza kufuatia ofa iliyokuwa mkononi mwake mara baada ya mkataba na Chelsea kufikia kikomo mwezi uliopita.
Beki huyo mwenye umri wa miaka 33, ameongeza kuwa baada ya kupewa taarifa hizo, mipango mbalimbali ilifanywa na alivutiwa na ukarimu wa viongozi pamoja na wafanyakazi wa AS Roma baada ya kufanya nao mawasilino siku chache kabla ya kufanya maamuzi.
Katika hatua nyingine Ashely Cole amesisitiza kutohofia suala la ubaguzi wa rangi atakapokuwa nchini Italia akiitumikia klabu ya AS Roma kwa kusema, sakata hilo kwa sasa ameshalizoea.
Amesema amewahi kukutana nalo mara kadhaa na ameona ni jambo ambalo haliwezi kumalizwa kwa mara moja, hata kama adhabu kali zitachukuliwa kwa wahusika ambalo siku zote wamekua hawapendezwi na watu wenye asili ya bara la Afrika.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

273838

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi