Home »
siasa afrika
» HII NDO TAHADHARI AMBAYO SHIRIKA LA KUTETEA HAKI ZA BINADAMU LA HUMAN RIGHTS WATCH IMEITOWA KUTOKANA NA UTUMIAJI WA WATOTO VITANI.
HII NDO TAHADHARI AMBAYO SHIRIKA LA KUTETEA HAKI ZA BINADAMU LA HUMAN RIGHTS WATCH IMEITOWA KUTOKANA NA UTUMIAJI WA WATOTO VITANI.
Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch
limetahadharisha katika ripoti yake juu ya kuongezeka utumikishwaji wa
watoto vitani huko Sudan Kusini. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mwenendo wa
watoto wanaotumiwa kama askari vitani umeongezeka katika nchi hiyo
changa zaidi barani Afrika kufuatia mapigano yanayoendelea kati ya
vikosi vya serikali ya Juba na waasi wanaoongozwa na Riek Machar
aliyewahi kuwa Makamu wa Rais. Shirika la Human Rights Watch limeitaka
serikali ya Sudan Kusini kuwarejesha katika familia zao watoto wote
ambao wanatumiwa na jeshi la serikali kama askari vitani. Kuwatumia
watoto vitani kama askari ni jambo lisilofaa kwa mujibu wa sheria za
Sudan Kusini na hata sheria za kimataifa.
Machafuko ya Sudan Kusini
ambayo yalianza Disemba mwaka jana, hadi sasa yamesababisha maelfu ya
watu kuuawa. Aidha zaidi ya watu milioni moja na nusu wamekuwa wakimbizi
kufuatia mapigano hayo. Suala la kuwatumia watoto kama askari vitani
linalofanywa na jeshi na waasi haliishii katika nchi ya Sudan Kusini
pekee; suala hilo limeenea katika nchi nyingi ambazo zinakabaliwa na
machafuko barani Afrika. Mbali na Sudan Kusini, kuna nchi kama Jamhuri
ya Kidemokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Chad, Somalia,
Zimbabwe, Sudan na Uganda ambazo suala la kuwafanya watoto askari ni
jambo la kawaida na lililoenea baina ya waasi na vikosi vya majeshi ya
serikali. Katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo waasi wanaofungamana
na makundi mbalimbali wamekuwa wakishambulia miji na vijiji tofauti vya
nchi hiyo ambapo baada ya kuwateka nyara watoto, baadaye huwatumikisha
watoto hao kama wapiganaji. Watoto hao mbali na kufanywa askari,
hutumiwa pia katika masuala mbalimbali kama ya ulinzi, ujasusi, utumwa
na propaganda vitani. Nchini Burundi pia kuna mamia ya watoto katika
makundi ya waasi yanayojihusisha na harakati za kijeshi. Aidha inaelezwa
kwamba, watoto wamekuwa wakitumiwa pia katika jeshi la Burundi. Kuenea
utumiwaji vibaya watoto barani Afrika kunaendelea kufanyika katika hali
ambayo, kuna mikataba mbalimbali iliyopasishwa kwa ajili ya kuzuia
watoto kushiriki katika vita. Kwa mujibu wa kipengee namba 38 cha
Mkataba wa Haki za Watoto, makundi ya kisiasa hayapaswi kuwatumia vitani
watu wenye umri wa chini ya miaka 15. Aidha kwa mujibu wa Protokali ya
Hiari ya Kushiriki Watoto Vitani, pande zinazopigana zinatakiwa
kutowaruhusu kushiriki katika vita watu walio na umri wa chini ya miaka
18 na kwamba, kuwachukua kwa nguvu watu hao na kuwafanya askari ni jambo
lililopigwa marufuku. Madola ya Magharibi yanaonesha kusikitishwa na
vitendo vya kuongezeka utumiaji watoto kama askari barani Afrika. Hata
hivyo hatua ya viongozi wa Magharibi ya kulaani utumiaji mabavu na
kutumiwa watoto vitani inatathminiwa na wajuzi wa mambo kwamba, kwa nia
ya kipropaganda, lengo likiwa ni kuzihadaa fikra za walio wengi
ulimwenguni. Mashirika ya kigeni barani Afrika yamekuwa yakiunga mkono
kuendelea machafuko katika nchi za bara hilo na hata yenyewe yanatajwa
kuwa chanzo halisi cha machafuko hayo.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
0 comments:
Toa Maoni yako
Tuambie Unafikilia Nini..!