Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » , » KAMA ULIKUWA HAUJUI BASI HIKI NDICHO ALICHO KISEMA COACH WA MANCHESTER CITY KUHUSIANA NA KUREJEA KWA MKALI BALOTELLI UINGEREZA.

KAMA ULIKUWA HAUJUI BASI HIKI NDICHO ALICHO KISEMA COACH WA MANCHESTER CITY KUHUSIANA NA KUREJEA KWA MKALI BALOTELLI UINGEREZA.

Written By Unknown on Monday 25 August 2014 | Monday, August 25, 2014

Kurejea kwa mshambuliaji kutoka nchini Italia Super Mario Barwuah Balotelli katika ligi ya nchini Uingereza baada ya kusajiliwa na majogoo wa jiji Liverpool, hakujamshtua meneja wa klabu bingwa nchini humo Manuel Luis Pellegrini Ripamonti.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliokuwa na mlengo wa mchezo wa hii leo, Manuel Pallegrini amesema hatua ya kurejea kwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24, anaichukulia kama ilivyo usajili wa wachezaji wengine waliojiunga na klabu zinazoshiriki ligi ya nchini Uingereza.
Amesema hakuna asiyejua Balitelli alikuwepo Man city na kisha alirejea nyumbani kwao Italia na akajiunga na AC Milan na sasa amerejea tena nchini Uingereza, hivyo kwa nini ichukuliwe kama ni mshangao kwake? Alihoji mzee huyo kutoka nchini Chile.

Pellegrini pia akaizungumzia tabia ya Mario Balotelli kwa kuwaeleza waandishi wa habari kwamba anamfahamu vyema na amekuwa na wasifu wa kipekee hivyo haoni la ajabu zaidi.
Ikumbukwe kuwa hii leo ligi ya nchini Uingereza itaendelea tena kwa mchezo mmoja ambapo Man city watakuwa nyumbani Etihad Stadium wakicheza dhidi ya majogoo wa jiji Liverpool waliomrejesha Super Mario Barwuah Balotelli nchini Uingereza kwa ada ya uhamisho wa paund million 16 akitokea AC Milan ya nchini Italia.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi